Uponyaji na Ukombozi kwa Damu ya Yesu.

Thursday, August 31, 2017

SOMO: NEEMA YA BWANA YESU.

NEEMA ni ya Bwana YESU, UPENDO ni wa Mungu BABA na USHIRIKA ni wa ROHO MTAKATIFU.
NEEMA ni Nini? Neema ni kitu ambacho mtu Anaweza kukipata pasipo kustahili. Tumeokolewa kwa Neema, sisi tulikuwa ni wenye dhambi na wala hatukustahili kuokolewa, lakini kwa Neema ya Bwana YESU tumepata kuokolewa.
Kwa nini Neema? Neema ndiyo inayokufungulia ili uweze kufika mahali ambapo utakuwa na SHUKRANI kwa Mungu, bila Neema huwezi kuwa na SHUKRANI. Kwa nini mtu mwenye Neema anakuwa na Shukrani? Ni kwa sababu ametendewa kitu ambacho hakutarajia kukipata. Jambo lolote ambalo unalipata pasipo tarajio na likakupa wewe Ahueni, Nafuu au Faraja hiyo ndiyo inaitwa NEEMA.
Neema ni ya muhimu sana kwa mtu yeyote yule Anayetamani kwenda mbele, awe ameokoka au hajaokoka, mtu akishafikiwa na Neema anakuwa na Changamko katika Maisha yake na SHUKRANI kwa Mungu wake, bila NEEMA hakuna Changamko wala Shukrani.
ITAMANI NEEMA KATIKA MAISHA YAKO ILI UWEZE KUWA BORA.
:- MTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA, EFATHA MINISTRY.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Facebook

Kuhusu Efatha

EFATHA.
EFATHA
maana yake ni Funguka [MARKO 7:34], Efatha ni huduma iliyo chini ya Mtume na Nabii JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA,Huduma ilianzishwa mwaka 1997.

Huduma ya Efatha mkoa wa Ruvuma inaongozwa na Mchungaji kiongozi PHILIPO JAMES GUNI, Katika Mkoa wa Ruvuma Huduma ya Efatha inapatikana Songea eneo la Mkuzo na Wilaya zote za Mkoa wa Ruvuma.
Huduma ya Efatha Ruvuma chini ya Mchungaji kiongozi PHILIPO JAMES GUNI,Tunatoa Huduma ya Uponyaji na Ukombozi kwa damu ya Yesu, Uponyaji na Ukombozi katika Magonjwa,Kipato, Kazi, Mazingira, Utasa, Ugumba, Uchumi ulioyumba, Umaskini, Ndoa, Kuachwa, Kuachika, Kukataliwa na mengine yote yaliyoshindikana, Huduma inatolewa bureee kwa damu ya YESU.
RATIBA ZETU ZA IBADA NI KAMA IFUATAVYO:
1.JUMATATU-IJUMAA –NI USHAURI NA MAOMBEZ, I Muda wote.
2.JUMAMOSI-IBADA YA MAOMBI, kuanzia saa 3:00 asubuhi-saa 6;00 mchana
3.JUMAPILI-IBADA KWA WATU WOTE, kuanzia saa 4:00 asubuhi- saa 8:00 mchana
Tunapatikana SONGEA-MKUZO, Kufika panda magari yaendayo MKUZO/MWENGEMSHINDO yanayopaki stendi kuu ya daladala Songea, shuka kituo kinachoitwa EFATHA uliza kanisa lililopo sio mbali kutoka barabarani.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Archive

Labels