KUTOKA MWENGE.
MCHUNGAJI ABIGAEL.
Zaburi 51: 1-3 “Ee Mungu, unirehemu, Sawasawa na fadhili zako. Kiasi cha wingi wa rehema zako, Uyafute makosa yangu. Unioshe kabisa na uovu wangu, Unitakase dhambi zangu. Maana nimejua mimi makosa yangu Na dhambi yangu i mbele yangu daima. ”
Yako mambo mengi ambayo wanadamu tunafanya ambayo hayampendezi Mungu lakini tunakuja mbele zake na kujifariji kana kwamba hakuna tulicho kosea badala ya kumlilia Mungu ili tuweze kupata huruma zake. Ukijua kuwa kuna jambo ambalo si zuri umelifanya usijifanye kama hujui bali unapaswa kutubu na kuacha.
Kanuni ya Mungu; Unapotenda dhambi au kukosea usimkimbie Mungu bali unapaswa kumkimbilia YEYE naye atakuosha na kukusafisha dhambi zako nawe utakuwa safi, usiwe na moyo mgumu, yatupasa kuacha uovu ili tuwe na furaha mbele za Mungu.
Ni mambo mangapi umefanya yasiyo mazuri mbele za Mungu na ukajifariji?, Hebu kubali kutubu na kuachana na uovu ulio kukamata ili uwe na FURAHA mbele za Bwana.
Lazima tukubali kuachana na dhambi ili tuweze kupokea kutoka kwa Mungu.
Lazia tutubu mbele za Mungu na si kujipaka mafuta wakati tu wachafu.
Zaburi 51: 1-3 “Ee Mungu, unirehemu, Sawasawa na fadhili zako. Kiasi cha wingi wa rehema zako, Uyafute makosa yangu. Unioshe kabisa na uovu wangu, Unitakase dhambi zangu. Maana nimejua mimi makosa yangu Na dhambi yangu i mbele yangu daima. ”
Yako mambo mengi ambayo wanadamu tunafanya ambayo hayampendezi Mungu lakini tunakuja mbele zake na kujifariji kana kwamba hakuna tulicho kosea badala ya kumlilia Mungu ili tuweze kupata huruma zake. Ukijua kuwa kuna jambo ambalo si zuri umelifanya usijifanye kama hujui bali unapaswa kutubu na kuacha.
Kanuni ya Mungu; Unapotenda dhambi au kukosea usimkimbie Mungu bali unapaswa kumkimbilia YEYE naye atakuosha na kukusafisha dhambi zako nawe utakuwa safi, usiwe na moyo mgumu, yatupasa kuacha uovu ili tuwe na furaha mbele za Mungu.
Ni mambo mangapi umefanya yasiyo mazuri mbele za Mungu na ukajifariji?, Hebu kubali kutubu na kuachana na uovu ulio kukamata ili uwe na FURAHA mbele za Bwana.
Lazima tukubali kuachana na dhambi ili tuweze kupokea kutoka kwa Mungu.
Lazia tutubu mbele za Mungu na si kujipaka mafuta wakati tu wachafu.
0 comments:
Post a Comment