Uponyaji na Ukombozi kwa Damu ya Yesu.

Sunday, November 26, 2017

SOMO: TOBA

KUTOKA MWENGE.
MCHUNGAJI ABIGAEL. 
Zaburi 51: 1-3 “Ee Mungu, unirehemu, Sawasawa na fadhili zako. Kiasi cha wingi wa rehema zako, Uyafute makosa yangu. Unioshe kabisa na uovu wangu, Unitakase dhambi zangu. Maana nimejua mimi makosa yangu Na dhambi yangu i mbele yangu daima. ”
Yako mambo mengi ambayo wanadamu tunafanya ambayo hayampendezi Mungu lakini tunakuja mbele zake na kujifariji kana kwamba hakuna tulicho kosea badala ya kumlilia Mungu ili tuweze kupata huruma zake. Ukijua kuwa kuna jambo ambalo si zuri umelifanya usijifanye kama hujui bali unapaswa kutubu na kuacha.
Kanuni ya Mungu; Unapotenda dhambi au kukosea usimkimbie Mungu bali unapaswa kumkimbilia YEYE naye atakuosha na kukusafisha dhambi zako nawe utakuwa safi, usiwe na moyo mgumu, yatupasa kuacha uovu ili tuwe na furaha mbele za Mungu.
Ni mambo mangapi umefanya yasiyo mazuri mbele za Mungu na ukajifariji?, Hebu kubali kutubu na kuachana na uovu ulio kukamata ili uwe na FURAHA mbele za Bwana.
Lazima tukubali kuachana na dhambi ili tuweze kupokea kutoka kwa Mungu.
Lazia tutubu mbele za Mungu na si kujipaka mafuta wakati tu wachafu.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Facebook

Kuhusu Efatha

EFATHA.
EFATHA
maana yake ni Funguka [MARKO 7:34], Efatha ni huduma iliyo chini ya Mtume na Nabii JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA,Huduma ilianzishwa mwaka 1997.

Huduma ya Efatha mkoa wa Ruvuma inaongozwa na Mchungaji kiongozi PHILIPO JAMES GUNI, Katika Mkoa wa Ruvuma Huduma ya Efatha inapatikana Songea eneo la Mkuzo na Wilaya zote za Mkoa wa Ruvuma.
Huduma ya Efatha Ruvuma chini ya Mchungaji kiongozi PHILIPO JAMES GUNI,Tunatoa Huduma ya Uponyaji na Ukombozi kwa damu ya Yesu, Uponyaji na Ukombozi katika Magonjwa,Kipato, Kazi, Mazingira, Utasa, Ugumba, Uchumi ulioyumba, Umaskini, Ndoa, Kuachwa, Kuachika, Kukataliwa na mengine yote yaliyoshindikana, Huduma inatolewa bureee kwa damu ya YESU.
RATIBA ZETU ZA IBADA NI KAMA IFUATAVYO:
1.JUMATATU-IJUMAA –NI USHAURI NA MAOMBEZ, I Muda wote.
2.JUMAMOSI-IBADA YA MAOMBI, kuanzia saa 3:00 asubuhi-saa 6;00 mchana
3.JUMAPILI-IBADA KWA WATU WOTE, kuanzia saa 4:00 asubuhi- saa 8:00 mchana
Tunapatikana SONGEA-MKUZO, Kufika panda magari yaendayo MKUZO/MWENGEMSHINDO yanayopaki stendi kuu ya daladala Songea, shuka kituo kinachoitwa EFATHA uliza kanisa lililopo sio mbali kutoka barabarani.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Archive

Labels