Uponyaji na Ukombozi kwa Damu ya Yesu.

Sunday, November 26, 2017



MTUMISHI WA MUNGU MTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA.
2Wafalme 4:18-37 “Hata yule mtoto alipokua, ikawa siku moja alitoka kwenda kwa baba yake kwenye wavunao. Akamwambia baba yake, Kichwa changu! Kichwa changu! Naye akamwambia mtumishi wake, Mchukue kwa mama yake. Akamchukua, akampeleka kwa mama yake, naye akakaa magotini mwake hata adhuhuri, kisha akafa………..” 
Watu wengi hapa Duniani wako katika mazingira haya inawezekena ukawa ni wewe, huyu mwanamke mshunami ambaye mtoto wake alikufa, alijitambu hivyo akasema kuwa hahitaji kulia. Alijua kuwa mtoto alitoka kwa Mungu hivyo akajua kuwa Mungu anaweza kufanya jambo kwa ajili ya mtoto wake. 
Yule mtoto alikuwa amekufa lakini yule mwanamke alikataa kulia na kukubaliana na ile hali ya kifo cha mtoto wake, alijua wapi pa kwenda maana alijua kuwa mtoto alitoka kwa Mungu. Ndipo alipochukua punda na mjakazi na kumwambia kuwa afanye haraka ili kuwahi kwa Mtumishi wa Mungu. Unapotaka kitu kitokee kwako fanya haraka kuwahi kwenye uwepo wa Mungu, maana Mungu wetu si mvivu hivyo unapaswa kufanya haraka ukitaka kitu kutoka kwake.

Share:

0 comments:

Post a Comment

Facebook

Kuhusu Efatha

EFATHA.
EFATHA
maana yake ni Funguka [MARKO 7:34], Efatha ni huduma iliyo chini ya Mtume na Nabii JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA,Huduma ilianzishwa mwaka 1997.

Huduma ya Efatha mkoa wa Ruvuma inaongozwa na Mchungaji kiongozi PHILIPO JAMES GUNI, Katika Mkoa wa Ruvuma Huduma ya Efatha inapatikana Songea eneo la Mkuzo na Wilaya zote za Mkoa wa Ruvuma.
Huduma ya Efatha Ruvuma chini ya Mchungaji kiongozi PHILIPO JAMES GUNI,Tunatoa Huduma ya Uponyaji na Ukombozi kwa damu ya Yesu, Uponyaji na Ukombozi katika Magonjwa,Kipato, Kazi, Mazingira, Utasa, Ugumba, Uchumi ulioyumba, Umaskini, Ndoa, Kuachwa, Kuachika, Kukataliwa na mengine yote yaliyoshindikana, Huduma inatolewa bureee kwa damu ya YESU.
RATIBA ZETU ZA IBADA NI KAMA IFUATAVYO:
1.JUMATATU-IJUMAA –NI USHAURI NA MAOMBEZ, I Muda wote.
2.JUMAMOSI-IBADA YA MAOMBI, kuanzia saa 3:00 asubuhi-saa 6;00 mchana
3.JUMAPILI-IBADA KWA WATU WOTE, kuanzia saa 4:00 asubuhi- saa 8:00 mchana
Tunapatikana SONGEA-MKUZO, Kufika panda magari yaendayo MKUZO/MWENGEMSHINDO yanayopaki stendi kuu ya daladala Songea, shuka kituo kinachoitwa EFATHA uliza kanisa lililopo sio mbali kutoka barabarani.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Archive

Labels