Uponyaji na Ukombozi kwa Damu ya Yesu.

Sunday, September 24, 2017

Vipo vizuizi vitano vinavyozuilia watu ulimwenguni kama

1. Kizuizi kinachohusika na uhuru wako
Umezaliwa ili uweze kufurahia baraka za Mungu na pia uweze kurithi vitu vyote vilivyomo katika ulimwengu huu.
Mwanadam amepungukiwa uwezo na nguvu wa kuweza kumiliki vitu vyote vilivyo katika ulimwengu huu ni lazima mwanadam akubali kulipa gharama ya kukipata alichotarajia au anachotarajia kukipata.
Wote waliookoka hutafutwa sana na shetani, ili kujiweka huru na salama ni lazima usimame imara kupigania haki pamoja na kuulinda muujiza ulioupata, maana unaposhindwa kuulinda muujiza ulioupata shetani atakupokonya au kuuharibu.
#ZINGATIA: Unapopata pata muujiza usimnyamazie Mungu, zidi kumsihi Mungu akupe neema ya kuutunza huo muujiza ulio upokea.
Amen....
Na Mchungaji Kiongozi Philipo James Guni.

Share:

MUENDELEZO WA SOMO LILIPITA: KIZUIZI

MCHUNGAJI KIONGOZI PHILIPO JAMES GUNI
Kizuizi ni uzio au ukuta unaokuzulia kuyafikia mabadiliko yako katka maendeleo yako .
Wengi miongoni mwa waliookoka baraka zao zipo nje na wao wapo ndani.
Wengi waliookoka hawajafanikiwa kwa kumiliki baraka zao katika wokovu.
Vizuizi vinaweza kukuzuia katika sehemu tofauti tofauti kama maendeleo yako, biashara yako, afya yako ya kimwili na kiroho.
Share:

Friday, September 22, 2017


Kuna kitu kikubwa Bwana Yesu analazimika kukifanya kwako.Anataka kukupa amani na tumaini lililopotea kulirejesha upya. Kwake wewe ni wa thamani sana,tena anakupenda na kukuheshimu.Usipuuze ujumbe huu wengi wamepokea uponyaji kwa kuamini na kuupokea ujumbe tu Comment_nimepokea_kwa_jina_la_Yesu_kisha_like_share
Share:

Sunday, September 17, 2017

Haleluya watumishi wa Bwana, karibuni katika Ibada za Jumapili ya leo hapa Efatha Ministry na katika vituo vyetu vyote vya Efatha Ministry ndani na nje ya nchi.
Kama uko mbali usikose kufuatilia Ibada hizi kupitia ukurasa huu wa Facebook , TRENET TV na katika Internet
Kusikiliza: www.mixlr.com/efatha-ministry 
YouTube: https://youtu.be/jS0ZoZDsV6s
Share:

Matukio kabla ya ibada.

Wana wa Mungu wakimsubiri na kumpokea Mchungaji kiongozi philipo James Guni.



Share:

Saturday, September 9, 2017

KUKUBALI.


Unahitaji kusikia Neno la Kristo linalohubiriwa na Manabii, Mitume na Watumishi wote wa Mungu, na baada kusikia kuna hatua inayofuata nayo ni KUKUBALI.
2 Nyakati 20:20 “Wakaamka asubuhi na mapema, wakaenda nje katika jangwa la Tekoa; nao walipokuwa wakitoka, Yehoshafati akasimama, akasema, Nisikieni, enyi Yuda nanyi wenyeji wa Yerusalemu; mwamini Bwana, MUNGU wenu, ndivyo mtakavyothibitika waaminini MANABII wake, ndivyo mtakavyo fanikiwa.”
Unahitajika KUKUBALI yale yote yanayohusiana na Ufalme wa Mungu, kwa sababu Mungu ana mpango wa KUKUTHIBITISHA. Mafanikio hayaji kama Mungu HAJAYAPITISHA, Mibaraka haimfikii mtu yeyote tu isipokuwa yule ambaye Mungu amemuwekea MUHURI wake ya kwamba huyo ABARIKIWE.
Mimi na wewe tunapaswa kukubali ya kwamba yule aliyetuwekea Ahadi nyingi katika Maisha yetu anataka KUZITHIBITISHA kwetu lakini YEYE Atazithibitisha kwa yule ambaye AMESIKIA NENO lake na KUKUBALI kile alicho KISIKIA, mtu huyo ukawe ni wewe kwa jina la YESU, Amen; UKATHIBITISHE KUPITIA NENO HILI.
Kwa nini unatakiwa Kukubali Habari za Ufalme wa Mungu unao hubiriwa? Kwa sababu unahitajika kuyabeba Mafanikio ya Ufalme wa Mungu.
Katikati ya watu wanao mtambulisha Mungu huku duniani wenye kuyabeba MAFANIKIO ni watu wachache sana. Kwa nini? Kwa sababu wengine WAMESIKIA lakini wamegoma kukubaliana na kile ambacho WAMEKISIKIA, hivyo hawawezi kupokea AHADI ambazo Mungu ameziahidi katika Maisha yao.
MUNGU akakujalie wewe kukubali kwa sababu YEYE Amekupa kuyabeba MAFANIKIO katika UFALME wake.

 Mchungaji Kiongozi Philipo James Guni, EFATHA MINISTRY- RUVUMA.

Share:

Sunday, September 3, 2017

Ukiwa katika kusubiria Muujiza wako lazima

1. Majaribu yaambatane nawe. Lazima uelewe wakati unasubiria muujiza wako majaribu ni lazima, usikwepe lazima ujaribiwe/upimwe je unaweza kupewa hicho ambacho unakisubiria.
Ukiwa katika kujaribiwa unapaswa kufanya yafuatayo:
-Kiri hicho ambacho unaamini.
Ayubu 23:10
2. Lazima utapitia mabaya.
Ukiona watu wanakutenga, wanakusema, hali ya msongo wa mawazo, hali ya kukata tamaa ujue upo katika msimu wa kusubiria muuijza wako.
3. Lazima utapitia kukatiswa tamaa.

unatakiwa kufanya nini ukiwa katika kusubiri?
1. Mwamini Mungu toka ndani ya moyo wako kuwa Mungu anaweza kufanya katika hilo unasubiria.

2. Soma neno la Mungu na kulishika.

3. Usiache kumkumbusha Bwana katika kile ambacho Mungu amekuahidi.
Isaya 62:6
Mtumishi wa Mungu Noel Michael Kapinga
Share:

MSIMU WA KUSUBIRI. (WAITING SEASON).

MSIMU WA KUSUBIRI. (WAITING SEASON).
Hauwezi kusubiri pasipo AHADI
Inaanza ahadi ndio panafuata kusubiri
Kuna msimu wa kupata na kuna msimu wa kusubiri, ukiwa katika kusubiri unahitaji
1. Uwe na tumaini.
2. Lazima uwe na Imani ukikosa Imani utakosa kile ambacho unasubiria, watu wengi wameshindwa kupokea ni kwa sababu ya kukosa Imani.
3. Lazima uwe mwaminifu.
Ukikosa uaminifu katika kusubiri Mungu anakasirika, na kile ambacho unakisubiria kinaondoka.
Kuwa mwaminifu katika muda, mali, fedha, katika hicho ambacho Mungu amekuandalia au amekupa.
4. lazima uwe na nguvu ya Mungu katika kusubiri.(Ayubu 6:11)
Lazima uwe na nguvu katika hicho ambacho unasubiri ili uujue mwisho wa kusubiria kwako sio unasema tu Mungu atafanya.
Wakati wa kusubiria muujiza wako au Baraka zako ndio wakati wa Mungu kukuandaa, tambua katika hicho ambacho unakisubiria kukipata, tambua kuwa Mungu anakuandaa ili uweze kukaa katika hiyo sehemu ambayo unaitarajia, kazi unayotarajia, biashara unayotarjia, kampuni unayotarajia.
Ndio maana bibi harusi anaandaliwa ili aweze kwenda kwenye harusi hawezi kuondoka katika ya kuandaliwa lazima asubiri mpaka fundi amalize ndipo aondoke, ndivyo hivyo hata kwa Mungu wengi wenu Mungu anawaandaa lakini kabla haujakamilishwa unakimbia, kukimbia kwako kunaondoa Baraka ulizoandaliwa.
MTUMISHI WA MUNGU NOEL MICHAEL KAPINGA.
Share:

Saturday, September 2, 2017

Welcome to the 9th Annual Gathering 2017. All guests both local and international.

Share:

Facebook

Kuhusu Efatha

EFATHA.
EFATHA
maana yake ni Funguka [MARKO 7:34], Efatha ni huduma iliyo chini ya Mtume na Nabii JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA,Huduma ilianzishwa mwaka 1997.

Huduma ya Efatha mkoa wa Ruvuma inaongozwa na Mchungaji kiongozi PHILIPO JAMES GUNI, Katika Mkoa wa Ruvuma Huduma ya Efatha inapatikana Songea eneo la Mkuzo na Wilaya zote za Mkoa wa Ruvuma.
Huduma ya Efatha Ruvuma chini ya Mchungaji kiongozi PHILIPO JAMES GUNI,Tunatoa Huduma ya Uponyaji na Ukombozi kwa damu ya Yesu, Uponyaji na Ukombozi katika Magonjwa,Kipato, Kazi, Mazingira, Utasa, Ugumba, Uchumi ulioyumba, Umaskini, Ndoa, Kuachwa, Kuachika, Kukataliwa na mengine yote yaliyoshindikana, Huduma inatolewa bureee kwa damu ya YESU.
RATIBA ZETU ZA IBADA NI KAMA IFUATAVYO:
1.JUMATATU-IJUMAA –NI USHAURI NA MAOMBEZ, I Muda wote.
2.JUMAMOSI-IBADA YA MAOMBI, kuanzia saa 3:00 asubuhi-saa 6;00 mchana
3.JUMAPILI-IBADA KWA WATU WOTE, kuanzia saa 4:00 asubuhi- saa 8:00 mchana
Tunapatikana SONGEA-MKUZO, Kufika panda magari yaendayo MKUZO/MWENGEMSHINDO yanayopaki stendi kuu ya daladala Songea, shuka kituo kinachoitwa EFATHA uliza kanisa lililopo sio mbali kutoka barabarani.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Archive

Labels