Chini ya jua mwanadamu akikosa furaha, anakosa changamko la moyo.
Mwanadamu yeyote akipata furaha ambayo chanzo chake ni Kristo, atachangamka.
Yeyote aliyekosa furaha ana chuki, ni mtu wa kuchukiwa, atahuzunishwa na mke, na mume, na watoto.
Mtu mwenye furaha ya wokovu, hata akifiwa na mtu ampendae sana, akiwa na hakika afaye afa katika Bwana, atahuzunika kimwili tu, bali hatokuwa na huzuni katika moyo wake.
Mtu mwenye furaha ya wokovu hatasumbuliwa na maneno ya wakosaji.
0 comments:
Post a Comment