Uponyaji na Ukombozi kwa Damu ya Yesu.

Thursday, August 31, 2017

SOMO: NEEMA YA BWANA YESU.

NEEMA ni ya Bwana YESU, UPENDO ni wa Mungu BABA na USHIRIKA ni wa ROHO MTAKATIFU.
NEEMA ni Nini? Neema ni kitu ambacho mtu Anaweza kukipata pasipo kustahili. Tumeokolewa kwa Neema, sisi tulikuwa ni wenye dhambi na wala hatukustahili kuokolewa, lakini kwa Neema ya Bwana YESU tumepata kuokolewa.
Kwa nini Neema? Neema ndiyo inayokufungulia ili uweze kufika mahali ambapo utakuwa na SHUKRANI kwa Mungu, bila Neema huwezi kuwa na SHUKRANI. Kwa nini mtu mwenye Neema anakuwa na Shukrani? Ni kwa sababu ametendewa kitu ambacho hakutarajia kukipata. Jambo lolote ambalo unalipata pasipo tarajio na likakupa wewe Ahueni, Nafuu au Faraja hiyo ndiyo inaitwa NEEMA.
Neema ni ya muhimu sana kwa mtu yeyote yule Anayetamani kwenda mbele, awe ameokoka au hajaokoka, mtu akishafikiwa na Neema anakuwa na Changamko katika Maisha yake na SHUKRANI kwa Mungu wake, bila NEEMA hakuna Changamko wala Shukrani.
ITAMANI NEEMA KATIKA MAISHA YAKO ILI UWEZE KUWA BORA.
:- MTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA, EFATHA MINISTRY.
Share:

NEEMA

Kazi ya Neema ni kuondoa HUZUNI na MACHUNGU, usione mtu ana HUZUNI au MACHUNGU ukajua kuwa hana UPENDO, La! Anao lakini kuna kitu kimekosekana kwake ambacho ni NEEMA; akipata NEEMA changamko linatokea katika Maisha yake.
• NEEMA ikikosekana kwako maswali yanakuwa mengi juu yako, Mtu mwenye NEEMA huwa hakataliwi popote pale atakapokwenda.
• Ili uweze Kuchanua unahitaji NEEMA, ukiwa mwanaume ni lazima NEEMA izidi kwako ili uweze kusababisha jambo litokee katika Maisha na Familia yako kiujumla.
• NEEMA ndiyo inayokuhalalisha wewe uweze Kukubalika, pasipo NEEMA huwezi kukubalika mbele za Mungu wala wanadamu, hata ungefanya jambo JEMA au ZURI kiasi gani.
• Ukiwa mahali ambapo umekwama kabisa NEEMA ndipo inapojitokeza na kukupa Msaada, NEEMA ndiyo inayoleta usaidizi, ili uweze kusaidiwa unahitaji NEEMA.
• Ukikosa NEEMA hata kama una sura nzuri hakuna atakayekuhitaji Kukuoa au atakayekubali kuolewa na wewe, NEEMA ni ya MUHIMU sana katika Maisha yako.

Ukiwa na NEEMA ndipo UBORA wako unapoanza Kuonekana, pasipo NEEMA huwezi kuwa BORA. NEEMA ni ya MUHIMU sana kwa kila mtu ambaye yuko chini ya jua, ili aweze kutokeza mahali na aonekane kuwa Yeye ni mtu. Ukiwa na UPENDO na NEEMA unaweza kufanya jambo na UKAFANIKIWA, lakini ukiwa na UPENDO bila NEEMA hakuna kitu ambacho utakifanya na KIKAFANIKIWA.
NEEMA ni ya MUHIMU sana kwa kila anayetamani kwenda Mbele au Kufanikiwa.
:- MTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA EFATHA MINISTRY.
Share:

UHALISIA.

UHALISIA
Katika kuishi kwako tambua kuna watu wamepewa vipawa,karama na vipaji ,Mungu ndie kawa gawia,
Sasa basi ukiwabaini unatakiwa uwa tunze,uwafundishe na kuwaongoza kwa upendo na hekima ,na wao wafurahi kuongozwa na wewe, ili uje kuvuna matunda mema baadae, sio kuwakatisha tamaa,kumbuka Mungu amekukutanisha nao kwa kusudi, unajua mara nyingine sio rahisi wewe kujua kila kitu,wengi hapo ndio tunakwama.
Tuwafanye watu kufanya wanachotakiwa kufanya,tuwafanye watu kuwa wanavyotakiwa kuwa,waamini .
Barikiwa
Mtumishi wa Mungu Noely Kapinga.
Share:

Sunday, August 27, 2017

SHUHUDA
Naitwa Avelina Haule

Namshukuru Mungu sana sana, nilikuwa nasumbuliwa na magonjwa mengi mengi kama #kisukari, #presha, na #malaria sugu ambayo kila dawa ilikuwa ikidunda tangu mpaka mwaka 1999, nilikuwa mtu wa kungangania dini kwa kipindi chote huku nikizunguka huku na kule kwa waganga wa kienyeji, hospitali kwenye matambiko lakini sikupata neema ya kupona kwa kipindi chote hicho lakini namshukuru huyu Mungu tangu nimeingia hapa Efatha navuta pumzi nzuri sina ugonjwa tena maana ilifika mahali mpaka napelekwa hospital napumulia mashine na wakati mwingine hata kutembea nilikuwa siwezi lakini namshukuru huyo Mungu mimi sasa ni mzima na nimeachana na dini na kuachana na wenyekiti wa jumuiy
a niliyokuwa nikitumikia kwa muda wa miaka 15. 
Share:

Sunday, August 20, 2017

Sunday Service.

Sunday Service.
Walokole wengi wavivu kupokea,huwezi kupata mafanikio kwa njia ya kufunga na kuomba. Hautakaa ufanikiwe katika hicho ambacho ulipewa upokee kwa kuwekewa mikono na wapakwa mafuta wa Bwana isipokuwa kwa kukichochea hicho kipawa.
Neema ya Mungu ni kwaajili ya watoto wa wachanga wa Imani ya Kristo,
Neema ni haki ya walokole wote. Neema naweza kufananisha na mahitaji ya kila siku ambayo mzazi ama mlezi anahusika kutoa kwa watoto wake. Hapo nyuma kipindi Israeli inatembea kutoka Misri kwenda nchi ya Ahadi kwa muda wa miaka kumi walikuwa wakila chakula kutoka mbinguni kinachoitwa Mana. (Neema kwa kipindi kile tunaweza sema kama mana). Neema ni kwaajili ya kila mtu hapa chini ya jua.
Mtumishi wa Mungu Mchungaji Kiongozi Philipo James Guni.
Share:

USHUHUDA

Naitwa Noel Athuman
Namshukuru Mungu kupitia semina ya kitume na kinabii nimetendewa mambo mengi kupitia neno la mtumishi wa Mungu aliyesimama mara ya mwisho katika semina alitutangazia kuwa wiki linalofuata baada ya wiki hile ya semina tutapokea zawadi.
 Namshukuru Mungu nimepata zawadi ya mtaji maana ilifika mahali mtaji ulikuwa unaelekea kuisha.

Pia, Namshukuru Mungu kanipa zadi ya shamba na mbegu zake katika hilo shamba na pia kupitia neno hilohilo namshukuru Mungu nimepa kazi tatu kwa wakati mmoja. Pia namshukuru zipo zawadi nyingi nimepata siwezi kusema zote ila namshukuru Mungu katika hayo. 
Share:

Sunday, August 13, 2017

SENIOR PASTOR PHILIPO JAMES GUNI 

REWARD.

Reward is anything that people gives as part of identification or part of testifying on what he/she has minister.
It’s to give something to someone due to what he/she has done.
Philippian 3:13-14
If there is a person who is giving you a gift
 He has valued you and appreciated you.
It’s a sign and wonder’s that he/she respect you because you have done than others.
 You're identified for what you've done.

Share:

Sunday Service.

MCH. KIONGOZI PHILIPO JAMES GUNI.
THAWABU.
Thawabu ni kitu chochote ambacho mtu anapewa kama sehemu ya utambulisho au sehemu ya uthibitisho wa huduma aliyoitoa.
Ni kitu chochote apewacho mtu kutokana na kazi aliyoifanya.
Filipi 3:13-14.
Mtu anayetoa thawabu ni ishara ya kuonyesha
- Amekuheshimu au kukuthamini.
unaheshimika kwasababu umefanya zaidi ya wengine.
- Unatambulika kwa kile ambacho umefanya.
Share:

Friday, August 11, 2017

SOMO: USTAWI WA MWAMINI.

 
MCH KIONGOZI MKOA WA MWANZA : VICTOR MALAMLA.
SOMO: USTAWI WA MWAMINI.


Waraka wa tatu wa Yohana 1:2 
Mungu anataka kila mwamini astawi, Ustawi ni utoshelevu wa kila unachohitaji, au ni ile hali yakufanikiwa kibiashara , kiofisi, familia nk.
Ustawi ni ile hali yakuushinda umaskini, maana umaskini ni mateso tuupinge umaskini kwa nguvu zote, msimamizi wa umaskini ni shetani mwenyewe.
Laana ya umaskini ikimwandama mtu kumtoka ni kazi sana, kama roho ya umaskini haijashughulikiwa kwako kufanikiwa ni ndoto hata kama umeokoka. halooo


Share:

Sunday service





Huwezi kustawi kama sio mwaminifu katika matakatifu ya Mungu.
Matakatifu ya Mungu ni yapi?
Muda wote uliotengwa kwaajili ya Mungu.
Matoleo yako kwa Mungu.
Ahadi zako kwa Mungu.


Share:

Facebook

Kuhusu Efatha

EFATHA.
EFATHA
maana yake ni Funguka [MARKO 7:34], Efatha ni huduma iliyo chini ya Mtume na Nabii JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA,Huduma ilianzishwa mwaka 1997.

Huduma ya Efatha mkoa wa Ruvuma inaongozwa na Mchungaji kiongozi PHILIPO JAMES GUNI, Katika Mkoa wa Ruvuma Huduma ya Efatha inapatikana Songea eneo la Mkuzo na Wilaya zote za Mkoa wa Ruvuma.
Huduma ya Efatha Ruvuma chini ya Mchungaji kiongozi PHILIPO JAMES GUNI,Tunatoa Huduma ya Uponyaji na Ukombozi kwa damu ya Yesu, Uponyaji na Ukombozi katika Magonjwa,Kipato, Kazi, Mazingira, Utasa, Ugumba, Uchumi ulioyumba, Umaskini, Ndoa, Kuachwa, Kuachika, Kukataliwa na mengine yote yaliyoshindikana, Huduma inatolewa bureee kwa damu ya YESU.
RATIBA ZETU ZA IBADA NI KAMA IFUATAVYO:
1.JUMATATU-IJUMAA –NI USHAURI NA MAOMBEZ, I Muda wote.
2.JUMAMOSI-IBADA YA MAOMBI, kuanzia saa 3:00 asubuhi-saa 6;00 mchana
3.JUMAPILI-IBADA KWA WATU WOTE, kuanzia saa 4:00 asubuhi- saa 8:00 mchana
Tunapatikana SONGEA-MKUZO, Kufika panda magari yaendayo MKUZO/MWENGEMSHINDO yanayopaki stendi kuu ya daladala Songea, shuka kituo kinachoitwa EFATHA uliza kanisa lililopo sio mbali kutoka barabarani.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Archive

Labels