Uponyaji na Ukombozi kwa Damu ya Yesu.

Thursday, August 31, 2017

NEEMA

Kazi ya Neema ni kuondoa HUZUNI na MACHUNGU, usione mtu ana HUZUNI au MACHUNGU ukajua kuwa hana UPENDO, La! Anao lakini kuna kitu kimekosekana kwake ambacho ni NEEMA; akipata NEEMA changamko linatokea katika Maisha yake.
• NEEMA ikikosekana kwako maswali yanakuwa mengi juu yako, Mtu mwenye NEEMA huwa hakataliwi popote pale atakapokwenda.
• Ili uweze Kuchanua unahitaji NEEMA, ukiwa mwanaume ni lazima NEEMA izidi kwako ili uweze kusababisha jambo litokee katika Maisha na Familia yako kiujumla.
• NEEMA ndiyo inayokuhalalisha wewe uweze Kukubalika, pasipo NEEMA huwezi kukubalika mbele za Mungu wala wanadamu, hata ungefanya jambo JEMA au ZURI kiasi gani.
• Ukiwa mahali ambapo umekwama kabisa NEEMA ndipo inapojitokeza na kukupa Msaada, NEEMA ndiyo inayoleta usaidizi, ili uweze kusaidiwa unahitaji NEEMA.
• Ukikosa NEEMA hata kama una sura nzuri hakuna atakayekuhitaji Kukuoa au atakayekubali kuolewa na wewe, NEEMA ni ya MUHIMU sana katika Maisha yako.

Ukiwa na NEEMA ndipo UBORA wako unapoanza Kuonekana, pasipo NEEMA huwezi kuwa BORA. NEEMA ni ya MUHIMU sana kwa kila mtu ambaye yuko chini ya jua, ili aweze kutokeza mahali na aonekane kuwa Yeye ni mtu. Ukiwa na UPENDO na NEEMA unaweza kufanya jambo na UKAFANIKIWA, lakini ukiwa na UPENDO bila NEEMA hakuna kitu ambacho utakifanya na KIKAFANIKIWA.
NEEMA ni ya MUHIMU sana kwa kila anayetamani kwenda Mbele au Kufanikiwa.
:- MTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA EFATHA MINISTRY.
Share:

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment

Facebook

Kuhusu Efatha

EFATHA.
EFATHA
maana yake ni Funguka [MARKO 7:34], Efatha ni huduma iliyo chini ya Mtume na Nabii JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA,Huduma ilianzishwa mwaka 1997.

Huduma ya Efatha mkoa wa Ruvuma inaongozwa na Mchungaji kiongozi PHILIPO JAMES GUNI, Katika Mkoa wa Ruvuma Huduma ya Efatha inapatikana Songea eneo la Mkuzo na Wilaya zote za Mkoa wa Ruvuma.
Huduma ya Efatha Ruvuma chini ya Mchungaji kiongozi PHILIPO JAMES GUNI,Tunatoa Huduma ya Uponyaji na Ukombozi kwa damu ya Yesu, Uponyaji na Ukombozi katika Magonjwa,Kipato, Kazi, Mazingira, Utasa, Ugumba, Uchumi ulioyumba, Umaskini, Ndoa, Kuachwa, Kuachika, Kukataliwa na mengine yote yaliyoshindikana, Huduma inatolewa bureee kwa damu ya YESU.
RATIBA ZETU ZA IBADA NI KAMA IFUATAVYO:
1.JUMATATU-IJUMAA –NI USHAURI NA MAOMBEZ, I Muda wote.
2.JUMAMOSI-IBADA YA MAOMBI, kuanzia saa 3:00 asubuhi-saa 6;00 mchana
3.JUMAPILI-IBADA KWA WATU WOTE, kuanzia saa 4:00 asubuhi- saa 8:00 mchana
Tunapatikana SONGEA-MKUZO, Kufika panda magari yaendayo MKUZO/MWENGEMSHINDO yanayopaki stendi kuu ya daladala Songea, shuka kituo kinachoitwa EFATHA uliza kanisa lililopo sio mbali kutoka barabarani.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Archive