KUTOKA MWENGE.
MTUMISHI WA MUNGU MTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA.
Mathayo 14:22-27 “Mara akawalazimisha wanafunzi wake wapande chomboni na kutangulia mbele yake kwenda ng'ambo, wakati yeye alipokuwa akiwaaga mkutano. Naye alipokwisha kuwaaga makutano, alipanda mlimani faraghani, kwenda kuomba. Na kulipokuwa jioni, alikuwako huko peke yake. ….. ”
Yesu akawaambi wanafunzi wake nendeni mbele kule ambako aliwaagiza waende, lakini katikati ya safari YESU akatokea kutoka kule mlimani alikokuwa akiomba peke yake. Siku unapotaka kuomba mbele za Mungu haijalishi ni watu wangapi wamekaa kando yako unapaswa kuwa peke yako, Mungu anapenda watu ambao wako peke yao. Wasahau wale walio kando yako na ujitazame wewe mwenyewe. Usimwangalie mume/mke wako, au ndugu yako aliye kaa jirani yako bali jiangalie mwenyewe na utamwona Mungu leo.
Yesu alitoka kule Mlimani akiwa tayari KUDHIHIRISHA NGUVU za MUNGU, huwezi kupata NGUVU za MUNGU mpaka uwe Mlimani na ukiwa peke yako. Tamani uwe peke yako ukiwa mbele za Mungu.
Baada ya maombi yale Yesu akatoka akiwa na UDHIHIRISHO wa NGUVU za MUNGU, unapotoka Mlimani unakuwa na uhakika wa NGUVU za MUNGU. Baada ya Yesu kufika kwa wanafunzi wake “akawaambia, Jipeni moyo ni mimi; msiogope. Siku ya leo ninakwambia kuwa USIOGOPE maana kuna kitu kitakutokea katika maisha yako, jiandae kupokea muujiza wako.
Mathayo 14:22-27 “Mara akawalazimisha wanafunzi wake wapande chomboni na kutangulia mbele yake kwenda ng'ambo, wakati yeye alipokuwa akiwaaga mkutano. Naye alipokwisha kuwaaga makutano, alipanda mlimani faraghani, kwenda kuomba. Na kulipokuwa jioni, alikuwako huko peke yake. ….. ”
Yesu akawaambi wanafunzi wake nendeni mbele kule ambako aliwaagiza waende, lakini katikati ya safari YESU akatokea kutoka kule mlimani alikokuwa akiomba peke yake. Siku unapotaka kuomba mbele za Mungu haijalishi ni watu wangapi wamekaa kando yako unapaswa kuwa peke yako, Mungu anapenda watu ambao wako peke yao. Wasahau wale walio kando yako na ujitazame wewe mwenyewe. Usimwangalie mume/mke wako, au ndugu yako aliye kaa jirani yako bali jiangalie mwenyewe na utamwona Mungu leo.
Yesu alitoka kule Mlimani akiwa tayari KUDHIHIRISHA NGUVU za MUNGU, huwezi kupata NGUVU za MUNGU mpaka uwe Mlimani na ukiwa peke yako. Tamani uwe peke yako ukiwa mbele za Mungu.
Baada ya maombi yale Yesu akatoka akiwa na UDHIHIRISHO wa NGUVU za MUNGU, unapotoka Mlimani unakuwa na uhakika wa NGUVU za MUNGU. Baada ya Yesu kufika kwa wanafunzi wake “akawaambia, Jipeni moyo ni mimi; msiogope. Siku ya leo ninakwambia kuwa USIOGOPE maana kuna kitu kitakutokea katika maisha yako, jiandae kupokea muujiza wako.
0 comments:
Post a Comment