Naitwa mtumishi Rose Nkondola wa eneo la Sayuni, namshukuru Mungu kwa matendo yake makuu kwangu,
Jambo la kwanza, ninamshukuru Mungu kwa ibada ya jumapili iliyopita, ilikuwa ni ibada ya furaha ya wokovu. Baada ya neno, mchungaji aliita wagonjwa japo sikuwa naumwa popote lakini nilipita mbele na mchungaji alipokuwa akiomba kwa uchungu nikaanza kufunguliwa, nikaanza kuomba msamaha kwa Mungu kwa yale mabaya niliyomtenda na kisha nguvu ya Mungu ikanishukia, nikahamishiwa katika ulimwengu wa roho nikaanza kumsifu na kumshukuru Mungu kwa kunirejeshea furaha tele ya wokovu na kunipa nguvu tele ya kutenda kazi yake.
Jambo la pili, nilikuwa nasumbuliwa na mguu toka mwaka 2011, ambapo ulianza baada ya kuona kama mtu ananichoma na sindano kwenye goti, nilipokuwa natoka shambani nilisumbuka nao sana. Katika bada ya Jumamosi kabla ya kwenda kusanyiko mwaka huu, Mchungaji aliyekuwepo siku hiyo, alisema kila anayeumwa aweke mkono pale anapoumwa,na atapokea uponyaji hapohapo au uponyaji utamfuata popote atakapokuwa, nami nikaweka mkono kwenye goti lile, kisha nilipokuwa nyumbani nimelala nikaota mtu amekuja ghafla akaingia ndani ya goti, akachomoa spoku na sindano, na toka hapo maumivu yameisha.
Namshukuru sana Mungu kwa huruma yake ameniponya bure, namshukuru sana.
Jambo la pili, nilikuwa nasumbuliwa na mguu toka mwaka 2011, ambapo ulianza baada ya kuona kama mtu ananichoma na sindano kwenye goti, nilipokuwa natoka shambani nilisumbuka nao sana. Katika bada ya Jumamosi kabla ya kwenda kusanyiko mwaka huu, Mchungaji aliyekuwepo siku hiyo, alisema kila anayeumwa aweke mkono pale anapoumwa,na atapokea uponyaji hapohapo au uponyaji utamfuata popote atakapokuwa, nami nikaweka mkono kwenye goti lile, kisha nilipokuwa nyumbani nimelala nikaota mtu amekuja ghafla akaingia ndani ya goti, akachomoa spoku na sindano, na toka hapo maumivu yameisha.
Namshukuru sana Mungu kwa huruma yake ameniponya bure, namshukuru sana.
0 comments:
Post a Comment