Uponyaji na Ukombozi kwa Damu ya Yesu.

Sunday, November 19, 2017

SHUHUDA.

Naitwa mtumishi Rose Nkondola wa eneo la Sayuni, namshukuru Mungu kwa matendo yake makuu kwangu, 
Jambo la kwanza, ninamshukuru Mungu kwa ibada ya jumapili iliyopita, ilikuwa ni ibada ya furaha ya wokovu. Baada ya neno, mchungaji aliita wagonjwa japo sikuwa naumwa popote lakini nilipita mbele na mchungaji alipokuwa akiomba kwa uchungu nikaanza kufunguliwa, nikaanza kuomba msamaha kwa Mungu kwa yale mabaya niliyomtenda na kisha nguvu ya Mungu ikanishukia, nikahamishiwa katika ulimwengu wa roho nikaanza kumsifu na kumshukuru Mungu kwa kunirejeshea furaha tele ya wokovu na kunipa nguvu tele ya kutenda kazi yake.
Jambo la pili, nilikuwa nasumbuliwa na mguu toka mwaka 2011, ambapo ulianza baada ya kuona kama mtu ananichoma na sindano kwenye goti, nilipokuwa natoka shambani nilisumbuka nao sana. Katika bada ya Jumamosi kabla ya kwenda kusanyiko mwaka huu, Mchungaji aliyekuwepo siku hiyo, alisema kila anayeumwa aweke mkono pale anapoumwa,na atapokea uponyaji hapohapo au uponyaji utamfuata popote atakapokuwa, nami nikaweka mkono kwenye goti lile, kisha nilipokuwa nyumbani nimelala nikaota mtu amekuja ghafla akaingia ndani ya goti, akachomoa spoku na sindano, na toka hapo maumivu yameisha.
Namshukuru sana Mungu kwa huruma yake ameniponya bure, namshukuru sana.

Share:

0 comments:

Post a Comment

Facebook

Kuhusu Efatha

EFATHA.
EFATHA
maana yake ni Funguka [MARKO 7:34], Efatha ni huduma iliyo chini ya Mtume na Nabii JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA,Huduma ilianzishwa mwaka 1997.

Huduma ya Efatha mkoa wa Ruvuma inaongozwa na Mchungaji kiongozi PHILIPO JAMES GUNI, Katika Mkoa wa Ruvuma Huduma ya Efatha inapatikana Songea eneo la Mkuzo na Wilaya zote za Mkoa wa Ruvuma.
Huduma ya Efatha Ruvuma chini ya Mchungaji kiongozi PHILIPO JAMES GUNI,Tunatoa Huduma ya Uponyaji na Ukombozi kwa damu ya Yesu, Uponyaji na Ukombozi katika Magonjwa,Kipato, Kazi, Mazingira, Utasa, Ugumba, Uchumi ulioyumba, Umaskini, Ndoa, Kuachwa, Kuachika, Kukataliwa na mengine yote yaliyoshindikana, Huduma inatolewa bureee kwa damu ya YESU.
RATIBA ZETU ZA IBADA NI KAMA IFUATAVYO:
1.JUMATATU-IJUMAA –NI USHAURI NA MAOMBEZ, I Muda wote.
2.JUMAMOSI-IBADA YA MAOMBI, kuanzia saa 3:00 asubuhi-saa 6;00 mchana
3.JUMAPILI-IBADA KWA WATU WOTE, kuanzia saa 4:00 asubuhi- saa 8:00 mchana
Tunapatikana SONGEA-MKUZO, Kufika panda magari yaendayo MKUZO/MWENGEMSHINDO yanayopaki stendi kuu ya daladala Songea, shuka kituo kinachoitwa EFATHA uliza kanisa lililopo sio mbali kutoka barabarani.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Archive

Labels