Uponyaji na Ukombozi kwa Damu ya Yesu.

Sunday, November 26, 2017

KUTOKA MWENGE.
MCHUNGAJI HELLEN MWINGA.
Marko 11:24 “ Kwa sababu hiyo nawaambia, Yo yote myaombayo mkisali, aminini ya kwamba mnayapokea, nayo yatakuwa yenu. ”
Chochote unacho omba ukisali, amini kuwa umepokea, unatakiwa umuombe Mungu na si mwanadamu, kuna mambo mengi tunayo tamani kupokea na hatuwezi kwa sababu hatujui nani wa kumuomba, wakati mwingine tumekuwa wepesi kuwaeleza watu shida zetu badala ya kumwambia Mungu. Unapaswa kuwa makini katika maombi yako ili uweze kupokea.
Neno la Mungu linasema ukiwa na imani unauwezo wa kuuambia mlima huu ng’oka na itakuwa hivyo, Mlima ni nini? Ni chochote kinacho kuzuia usipite au usisonge mbele, hivyo ukiwa na imani unauwezo wa kukiambia hicho kinachokuzuia kiondoke na ikawa hivyo

Share:

0 comments:

Post a Comment

Facebook

Kuhusu Efatha

EFATHA.
EFATHA
maana yake ni Funguka [MARKO 7:34], Efatha ni huduma iliyo chini ya Mtume na Nabii JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA,Huduma ilianzishwa mwaka 1997.

Huduma ya Efatha mkoa wa Ruvuma inaongozwa na Mchungaji kiongozi PHILIPO JAMES GUNI, Katika Mkoa wa Ruvuma Huduma ya Efatha inapatikana Songea eneo la Mkuzo na Wilaya zote za Mkoa wa Ruvuma.
Huduma ya Efatha Ruvuma chini ya Mchungaji kiongozi PHILIPO JAMES GUNI,Tunatoa Huduma ya Uponyaji na Ukombozi kwa damu ya Yesu, Uponyaji na Ukombozi katika Magonjwa,Kipato, Kazi, Mazingira, Utasa, Ugumba, Uchumi ulioyumba, Umaskini, Ndoa, Kuachwa, Kuachika, Kukataliwa na mengine yote yaliyoshindikana, Huduma inatolewa bureee kwa damu ya YESU.
RATIBA ZETU ZA IBADA NI KAMA IFUATAVYO:
1.JUMATATU-IJUMAA –NI USHAURI NA MAOMBEZ, I Muda wote.
2.JUMAMOSI-IBADA YA MAOMBI, kuanzia saa 3:00 asubuhi-saa 6;00 mchana
3.JUMAPILI-IBADA KWA WATU WOTE, kuanzia saa 4:00 asubuhi- saa 8:00 mchana
Tunapatikana SONGEA-MKUZO, Kufika panda magari yaendayo MKUZO/MWENGEMSHINDO yanayopaki stendi kuu ya daladala Songea, shuka kituo kinachoitwa EFATHA uliza kanisa lililopo sio mbali kutoka barabarani.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Archive

Labels