Uponyaji na Ukombozi kwa Damu ya Yesu.

Sunday, September 3, 2017

MSIMU WA KUSUBIRI. (WAITING SEASON).

MSIMU WA KUSUBIRI. (WAITING SEASON).
Hauwezi kusubiri pasipo AHADI
Inaanza ahadi ndio panafuata kusubiri
Kuna msimu wa kupata na kuna msimu wa kusubiri, ukiwa katika kusubiri unahitaji
1. Uwe na tumaini.
2. Lazima uwe na Imani ukikosa Imani utakosa kile ambacho unasubiria, watu wengi wameshindwa kupokea ni kwa sababu ya kukosa Imani.
3. Lazima uwe mwaminifu.
Ukikosa uaminifu katika kusubiri Mungu anakasirika, na kile ambacho unakisubiria kinaondoka.
Kuwa mwaminifu katika muda, mali, fedha, katika hicho ambacho Mungu amekuandalia au amekupa.
4. lazima uwe na nguvu ya Mungu katika kusubiri.(Ayubu 6:11)
Lazima uwe na nguvu katika hicho ambacho unasubiri ili uujue mwisho wa kusubiria kwako sio unasema tu Mungu atafanya.
Wakati wa kusubiria muujiza wako au Baraka zako ndio wakati wa Mungu kukuandaa, tambua katika hicho ambacho unakisubiria kukipata, tambua kuwa Mungu anakuandaa ili uweze kukaa katika hiyo sehemu ambayo unaitarajia, kazi unayotarajia, biashara unayotarjia, kampuni unayotarajia.
Ndio maana bibi harusi anaandaliwa ili aweze kwenda kwenye harusi hawezi kuondoka katika ya kuandaliwa lazima asubiri mpaka fundi amalize ndipo aondoke, ndivyo hivyo hata kwa Mungu wengi wenu Mungu anawaandaa lakini kabla haujakamilishwa unakimbia, kukimbia kwako kunaondoa Baraka ulizoandaliwa.
MTUMISHI WA MUNGU NOEL MICHAEL KAPINGA.
Share:

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment

Facebook

Kuhusu Efatha

EFATHA.
EFATHA
maana yake ni Funguka [MARKO 7:34], Efatha ni huduma iliyo chini ya Mtume na Nabii JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA,Huduma ilianzishwa mwaka 1997.

Huduma ya Efatha mkoa wa Ruvuma inaongozwa na Mchungaji kiongozi PHILIPO JAMES GUNI, Katika Mkoa wa Ruvuma Huduma ya Efatha inapatikana Songea eneo la Mkuzo na Wilaya zote za Mkoa wa Ruvuma.
Huduma ya Efatha Ruvuma chini ya Mchungaji kiongozi PHILIPO JAMES GUNI,Tunatoa Huduma ya Uponyaji na Ukombozi kwa damu ya Yesu, Uponyaji na Ukombozi katika Magonjwa,Kipato, Kazi, Mazingira, Utasa, Ugumba, Uchumi ulioyumba, Umaskini, Ndoa, Kuachwa, Kuachika, Kukataliwa na mengine yote yaliyoshindikana, Huduma inatolewa bureee kwa damu ya YESU.
RATIBA ZETU ZA IBADA NI KAMA IFUATAVYO:
1.JUMATATU-IJUMAA –NI USHAURI NA MAOMBEZ, I Muda wote.
2.JUMAMOSI-IBADA YA MAOMBI, kuanzia saa 3:00 asubuhi-saa 6;00 mchana
3.JUMAPILI-IBADA KWA WATU WOTE, kuanzia saa 4:00 asubuhi- saa 8:00 mchana
Tunapatikana SONGEA-MKUZO, Kufika panda magari yaendayo MKUZO/MWENGEMSHINDO yanayopaki stendi kuu ya daladala Songea, shuka kituo kinachoitwa EFATHA uliza kanisa lililopo sio mbali kutoka barabarani.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Archive